Tumbo kujaa gesi na matibabu yake

Image result for stomach cramps"
Tumbo kujaa gesi ni tatizo linalowakumba watu wengi gesi inapojaa tumboni tumbo linaweza kuvimba,kuwa gumu na wakati mwingine kuuma kama vichomi.

Dalili za tumbo kujaa gesi

-Kutoa hewa mara kwa mara kupitia mdomoni (kubeua) au kwenye njia ya haja kubwa
-Kuwa na milio kama muziki ndani ya tumbo
-Tumbo kuwa kama limebanwa kiasi cha kusababisha kufungua mkanda au kulegeza nguo iliovaliwa
-Mara nyingine ni kutokana ma magonjwa kama figo,ini au moyo

Sababu za tumbo kujaa gesi

-Kula chakula kwa haraka huku mtu akiongea
-Uvutaji sigara
-Magonjwa na maambukizi katika mfumo wa chakula na hasa kwenye utumbo hali inayozuia kusagwa na kufyonzwa kwa chakula
-Kutumia vinywaji vyenye kaboneti (carbonates) nyingi kama vile cola na kula vyakula vyenye gesi mara kwa mara kama vile maharage,vitunguu na kabeji

Tiba yake

-Kunywa chai yenye tangawizi au karafuu kunasaidia kupunguza gesi
-Kutafuna mbegu za maboga kunasaidia kulainisha mfumo wa chakula
-Kufanya mazoezi mepesi ya kutembea na kurukaruka

Iwapo hatua za tiba binafsi hazitoi matunda inashauriwa muhusika aende hospitali kwa ushauri zaidi wa kitabibu.

Post a Comment

Previous Post Next Post