kwanini bangi yaidhinishwa na mataifa mengi kwa kasi?


Sehemu mbalimbali duniani mtazamo kuhusiana na matumizi ya mmea wa cannabis yaani bangi unabadilika kwa kasi.


Serikali mpya ya Mexico ina mpango wa kuhalalisha matumizi ya bangi kama njia ya kujiburudisha, sawa na ilivyofanya utawala mpya wa Luxembourg. Wakati huo huo, viongozi wakuu nchini New Zealand, wanakusudia kuandaa kura ya maoni ya namna watakavyoshughulikia swala hilo.
Jinsi maoni ya umma - na yale ya serikali- yanavyobadilika, ni dhahiri kuwa mataifa mengi yatafuata mkondo huo. Maswali yanayoibuka ni kwa namna gani nchi hizo zitadhibiti matumizi na usambazaji wa mmea huo?


Ni nini hasa kinachopelekea mataifa mbalimbali katika kulegeza kamba kwenye sheria zake, au hata kuamua kuidhinisha ,matumizi ya bangi moja kwa moja?
Vita dhidi ya mihadarati
Ilikuwa mwaka 2012 ambapo Uruguay, ilipoandika historia kwa kuwa taifa la kwanza duniani kuruhusu matumizi ya bangi kwa minajili ya kujiburudisha. Hatua hiyo, kwa uhalisia, ilikuwa na nia ya kuiwezehsa serikali kushughulikia biashara haramu na magenge ya wahalifu waliokuwa wanaiongoza biashara hiyo.
Baadaye mwaka huo, wapiga kura katika majimbo mawili ya Washington na Colorado, wakawa wa kwanza kabisa nchini Marekani kuunga mkono uidhinishwaji wa matumizi ya bangi ambayo si ya kimatibabu.
Chini ya utawala wa Barack Obama, msisitizo uliwekwa kwenye majimbo kuwa huru katika kubadili sheria zake za kuratibu matumizi ya bangi.
Majimbo manane mengine kwa pamoja na Washington DC, yameunga mkono uhalalishwaji wa bangi kwa njia ya kujiburudisha huku hukumu ya kupatikana au kutumia kama dawa ikilegezwa kwingineko.
Matumizi ya bangi kwa minajili ya dawa, sasa yanakubaliwa katika majimbo 33 kati ya majimbo 50 nchini Marekani.

BangiHaki miliki ya picha PA
Image caption
Uruguay na Canada wanaruhusu uvutwaji wa bangi hadharani
Sasa wimbi hilo limetanda kote Marekani na linakwenda kwa kasi mno, huku Canada ikihalalisha uuzaji, umiliki na matumizi ya bangi kwa njia ya kujiburudisha kote nchini humo mwezi Oktoba mwaka huu.
Kwa Mexico kuhalalisha bangi bila shaka ni jambo la hakika. Serikali mpya ya Andrés Manuel López Obrador imewasilisha muswada bungeni, ambao utahalalisha matumizi yake kama dawa na burudani, ilihali mahakama ya juu zaidi nchini humo, hivi majuzi iliamua kuwepo kwa marufuku ya matumizi ya bangi kwa njia ya burudani, kwamba ni kinyume cha sheria.
Mataifa mengine yanaongeza shinikizo. Ingawa uuzaji wa bangi unasalia kuwa haramu, kupatikana na kiwango kidogo sio tena uvunjaji wa sheria katika mataifa ya Brazil, Jamaica na Ureno.
Nchini Uhispania ni ruhusa kuvuta bangi japo kwa siri, ilihali dawa hizo zinauzwa wazi katika maduka yenye majina Coffee Shops nchini Uholanzi. Bado mataifa mengi yanakubalia matumizi ya cannabis kwa matibabu.
Nchini Uingereza, madaktari wamekubaliwa kuwapa wagonjwa bidhaa za cannabis tangu mwezi Novemba.Korea Kusini wamehalalisha matumizi ya bangi kama dawa lakini chini ya mazingira yenye sheria kali, licha ya kuwahukumu wakaazi wanaotumia dawa hizo hata nje ya nchi.

bangiHaki miliki ya picha Reuters
Hukumu ya kifo kwa mvulana mmoja aliyepatikana akiuza mafuta ya bangi, imesababisha mjadala mkali wa uhalalishaji wa bangi nchini Malaysia. Lebanon inadhamiria kuhalalisha uzalishaji wa cannabis kwa matibabu, na pia kusaidia kuboresha uchumi wa taifa.
Lesotho ilikuwa nchi ya kwanza Afrika kuruhusu kilimo na matumizi ya bangi kwa sababu za kiafya tu. Tayari wakulima wamegeukia zao hilo na wanapata pesa maradufu.
Mwezi Aprili mwaka huu, Zimbabwe ilikuwa nchi ya pili Afrika kuhalalisha uzalishaji wa bagi kwa matumizi ya kiafya na kisayansi.
Septemba mwaka huu Mahakama ya Kikatiba nchini Afrika Kusini ilihalalisha utumiaji wa bangi kwa watu wazima katika maeneo faragha.
Watoto wagonjwa
Mwanzo wa kuhalalisha bangi umekuwa ni huruma ya jamii. Nchini Marekani na Canada, picha za watoto ambao ni wagonjwa na uzima wao ni dawa zenye vimelea vya bangi zilitumika kufanya kampeni ya kuhalalisha bangi.
Canada iliruhusu matumizi ya bangi kimatibabu mwanzoni mwa miaka ya 2000 kabla ya kuruhusu kuwa kiburudisho mwaka huu.
Mtazamo kama huo pia umeshuhudiwa nchini Uingereza.
Mwezi Juni, Billy Gladwell mwenye umri wa miaka 12, aliyekuwa akiugua kifafa, alilazwa hospitalini, baada ya dawa yake mafuta ya bangi ilipokamatwa. Mwezi mmoja baadaye, leseni maalum ya kutumia mafuta ya bangi ikatolewa kwa Alfie Dingley mwenye umri wa miaka 7, aliyekuwa akiugua pia kifafa.

Alfie DingleyHaki miliki ya picha PA
Image caption
Mamake Alfie Dingley anasema mafuta ya cannabis imemsaidia mwanawe dhidi ya kifafa
Mwezi Juni, Billy Gladwell mwenye umri wa miaka 12, aliyekuwa akiugua kifafa, alilazwa hospitalini, baada ya dawa yake mafuta ya bangi ilipokamatwa. Mwezi mmoja baadaye, leseni maalum ya kutumia mafuta ya bangi ikatolewa kwa Alfie Dingley mwenye umri wa miaka 7, aliyekuwa akiugua pia kifafa.
Kufuatia kampeni ya nguvu, serikali ya Uingereza iliamua kubadilisha sheria ili kuwakubalia madaktari kuwapa wagonjwa matibabu yanayotokana na bidhaa za bangi.
Lakini nchini Uingereza, Wizara ya mambo ya ndani, inasema matumizi ya bangi kwa njia ya burudani, itasalia kupigwa marufuku, hata ingawa maafisa wakuu, akiwemo kiongozi mmoja mkuu wa chama cha Conservative, William Hague, akipendekeza hatua hiyo ifikiriwe upya.
Mexico pia ina kesi ya watoto wanaokatazwa kupewa bangi kwa matibabu, lakini pia inakabiliwa na changamoto ya ghasia zinazohusishwa na vita vya ulanguzi wa mihadarati.
Hata ingawa bangi ni sehemu ndogo mno ya asilimia kubwa ya magenge yanayojihusisha na uuzaji wa dawa za kulevya, marufuku dhidi yake inaonekana kuchochea zaidi kuongezeka kwake kuliko hali ilivyo.
Wanadiplomasia wa Mexico, wanaionya Marekani kuwa, ni vigumu mno kukabiliana na bangi huku jimbo jirani la California limeidhinisha matumizi yake.
Masoko ya Bangi

BangiHaki miliki ya picha Getty Images
Huku mataifa mengi duniani yakielekea katika hali ya kuleta mabadiliko ya uhalalishaji wa bangi, ni wazi soko la zao hilo litazidi kupanuka.
Serikali za nchi za Amerika ya Kusini zinataka wakulima wao kuyafikia masoko hayo ya biashara kubwa ya ukulima wa bangi kwa minajili ya matibabu, ambayo yanaszidi kukua kila uchao.
Nchini Lesotho, wakulima tayari wameanza kuvuna faida ya kilimo hicho.
Mashirika makubwa pia yameonyesha hitaji la kujiunga nayo. Kampuni ya Altria, ambayo ni wazalishaji wa chapa maarufu ya sigara za Marlboro wapo katika mazungumzo na kampuni moja ya kuzalisha bangi nchini Canada ili wawekeze mtaji wao wa dola bilioni 1.86.
Wazalishaji wa bia ya Corona, kampuni ya Constellation Brands imesema itawekeza dola bilioni 4 kwenye kampuni kubwa zaidi ya uzalishaji bangi nchini Cananda, Canopy Growth. Uwekezaji huo ndio mkubwa zaidi mpaka sasa katika biashara ya bangi duniani.
Kampuni maarufu ya vinywaji ya Coca-Cola ni maarufu zaidi kwa kutengeneza soda, lakini sasa inapanga kufanyia majaribio aina mpya ya kinywaji ambacho kitakuwa na bangi.
Changamoto kubwa kwa sasa, ni matumizi ya cannabis kwa burudani, haiwezi kuwa biashara kutoka taifa moja hadi nyingine. Mataifa tu yatanunua bidhaa hiyo kutoka nje au kuuza nje ya nchi kama tiba chini ya mfumo wa leseni inayopigiwa msasa na Bodi ya Kimataifa ya Kudhibiti Mihadarati.
Wakulima katika mataifa kama vile Morocco na Jamaica, wanasifika kwa kuzalisha bangi nzuri lakini hawataweza kuyafikia masoko ambayo wakulima wake wa ndani si wazuri kama ilivyotokea nchini Canada mara tu baada ya kuhalalisha.

Presentational grey line
Madhara ya Bangi
◾Unaweza kusababisha kuchanganyikiwa na wasiwasi usio wa kawaida
◾Ikivutwa na tumbaku, inaweza kuongeza hatari ya ugonjwa kama vile saratani ya mapafu
◾Matumizi ya mara kwa mara yamehusishwa na hatari ya kupatwa na magonjwa ya kiakili
◾Upungufu wa kudumu wa kiwango cha mtu kufikiria na kufahamu mambo, baada ya kutumia kwa muda mrefu

Post a Comment

Previous Post Next Post