Zifahamu dalili za usonji kwa watoto (autism)


Image result for autism



Usonji

Usonji ni hali ambayo ubongo unashindwa kufanya kazi ya kutambua mazingira kwa hiyo mtoto anakua kwenye mazingira yake yeye mwenyewe

Dalili za usonji kwa watoto(autism)

Mtoto kuonesha tabia tofauti na watoto wengine mfano anaweza kua pekeyake pekeyake au kwenye mazingira yake yeye mwenyewe
mtoto ataonesha tabia tofauti sana ukilinganisha na watoto wengine wa rika lake

Wataalam wanazungumzia nini kuhusu usonji?

Wataalam wanazungumza kua tatizo hili huwa lina gundulika mara nyingi mtoto anapofikia umri wa miaka mitatu

Je usonji unaweza kuutambua mapema?

Ndiyo,usonji unaweza kuutambua mapema hata mtoto akifikisha miezi sita ikiwa unamfuatilia kwa karibu

Je, utatambuaje kama mtoto amekumbwa na tatizo la usonji?

-Utakapokua unamnyonyesha anaweza akawa ananyonya kwa nguvu sana au anabana nyonyo sana
-Ukitaka kumvalisha au kumbadilisha nepi anaweza akawa mkali  sana
-Ukimgeuza tuu kidogo anaweza akalia sana
-Mtoto kwa kawaida anatakiwa kucheka akisha fikisha mwezi baada ya kuzaliwa,lakini mtoto ambaye anadalili za kuonesha usonji kucheka kwake huwa ni tabu sana au hata kuonesha kucheka kwake hua ni tabu sana
-Huonesha kukasirika sana
-Haoneshi mawasiliano kwa mama mfano wakati mama akitaka kucheza nae wakati anamyonyesha au kumbadilisha nguo
-Hizo ni dalili za awali ambazo unaweza kuzitambua ni kwa nini mtoto anakua mkali kwenye vitendo vya kawaida vya kila siku.
-Jinsi mtoto anavyokua ndivyo usonji unavyozidi kukua
-Inafika hatua mtoto kushindwa hata kuzungumza na ndio maana wataalamu husema kwamba usonji hugundulika kwa miaka mitatu kwa sababu ni kipindi ambacho mtoto anapaswa kuzungumza lakini mtoto mwenye usonji kufikia kipindi hiki cha miaka mitatu hua mara nyingi hushindwa kuzungumza
-Huchagua sana vyakula
-Wakati mwingine akianza kutembea hua anatembelea vidole tuu
-Hupenda kupanda sana juu ya vitu vilivyoinukaa mfano juu ya meza juu ya dirisha na akishapanda huganda hapo kwa muda mrefu bila kuachilia wala kudondoka
-Anaweza asiwajue anaoishi nao hata mama yake na baba yake au hata mazingira ya nyumbani huyapoteza kumbukumbu kwa haraka

Ni sehemu gani kwenye mwili huhusika sana na tatizo la usonji?

Ubongo huhusika sana na usonji kwa sababu hisia ndio chakula cha ubongo kwa sababu ili ubongo uweze kufanya kazi vizuri ni lazima hisia zinazofika kwenye ubongo ziwe nzuri yaani zisizoathirika zisiwe nyingi sana au kidogo sana kwa sababu hisia zinafanya kzi kwa uwiano ulio sawa

SABABU ZINAZOWEZA KUPELEKEA MTOTO KUWA NA USONJI

-Njaa kali
-Mama kua na msongo wa mawazo kipindi cha ujauzito

TIBA YA USONJI

-Mzazi unapaswa kua karibu sana na mtoto endapo utagundua tabia tofauti kwa mtoto wako
-Mpeleke mtoto kwenye kituo cha afya pindi tuu uonapo dalili za usonji
-Mzazi unapaswa kumruhusu mtoto kucheza ili kukuza milango yake ya fahamu
-Afya ya mama mjamzito inachangia kwa kiasi kikubwa kumlinda mtoto asikumbwe na usonji

Post a Comment

Previous Post Next Post