Kukabiliana na vidonda vya ulimi


What’s Causing My Sore Tongue?

Shida nyingi zinaweza kuathiri ulimi wako kama vile:
maumivu ,vidonda ,uvimbe ,mabadiliko katika ladha ,mabadiliko katika rangi

Dalili zifuatazo zinaweza kuashiria matatizo ya ulimi:
upotezaji wa ladha au sehemu kamili au mabadiliko katika uwezo wako wa kuonja tamu, uchungu,chachu au ladha tamu ,ugumu wa kusonga ulimi wako ,uvimbe wa ulimi,
mabadiliko kutoka kwa rangi ya kawaida ya ulimi wako au viraka vya rangi ambayo ni nyeupe, rangi nyekundu, nyeusi, au hudhurungi
maumivu yanaweza kua juu ya ulimi au katika sehemu kadhaa tu za ulimi wako

VIDONDA VYA ULIMI  ni michubuko inayotokea kwenye mdomo na ulimi. Vidonda hivi husababisha mhusika kupata maumivu kwa maana kinywa ni moja ya sehemu ya mwili yenye mishipa mingi ya fahamu na wakati mwingine vidonda katika kinywa husababisha kushindwa kuongea vizuri.

Ingawa vidonda hukufanya ujisikie vibaya, huwa vinapona vyenyewe ndani ya wiki moja au mbili. Vidonda vya kinywa hutokea kwenye au ndani ya mashavu, midomo (lips), ulimi, kingo na kuta za meno pia huweza kusambaa mpaka kwenye koromeo ikiwa havitatibiwa kwa wakati.
Vidonda vya mdomo huwa vya duara na hutokea ndani ya kinywa, kwenye ulimi na midomo. Vinaweza kuvimba na kuwa vyeupe, vyekundu au vya kijivu. Inawezekana kuwa na kidonda kimoja au zaidi wakati mmoja na kusambaa ndani ya kinywa.

Wakati Gani Unapaswa Kupata Msaada wa Kitabibu?
Vidonda mdomoni huwatokea watu wengi kwa kawaida na hupona bila ya matibabu ya daktari wa kinywa. Ikiwa vidonda vitatudumu zaidi ya wiki tatu, zungumza na daktari.
Ikiwa vidonda vitauma na vitakufanya ushindwe kula, kunywa au kusukutua meno. Ikiwa vidonda vinajirudiarudia, au vidonda vinapokuwa na maumivu zaidi au vyekundu kitu kinachoweza kuashiria maambukizi ya bacteria.
Vidonda kwenye kinywa vinaweza kuwa moja ya dalili ya ugonjwa unaosababishwa na virusi unaoathiri mikono, miguu na mdomo. Ugonjwa huathiri zaidi watoto chini ya miaka 10 wakati mwingine huathiri hata watu wazima.

Matibabu yanaweza kupunguza uvimbe na kuondoa wasiwasi. Vitu unavyoweza kufanya kuharakisha uponaji wa vidonda ni pamoja na
 kupaka dawa kwenye vidonda, kutumia mswaki laini kusukutua meno, ktumia dawa ya meno isiyo na sodium laryl sulphate ambayo inaweza kukereketa, kutotumia vyakula vyenye viungo vingi na chumvi nyingi.kula matunda na mboga za majani.

Nini Husababisha Vidonda kwenye Kinywa?

Mara nyingi chanzo cha vidonda kwenye kinywa si cha moja kwa moja. Mara nyingi kidonda kimoja kwenye kinywa husababishwa na uharibifu wa utando laini ndani ya kinywa kwa mfano unapojing’ata kwa bahati mbaya au unapokula chakula kigumu.

Haijulikani wazi ni nini husababisha vidonda kwenye kinywa ambavyo hujirudia mara kwa mara, lakini vitu vinavyochochea ni pamoja na msongo, wasiwasi, mabadiliko ya homoni, mfano, baadhi ya wanawake hupatwa na vidonda mdomoni wanapokuwa kwenye siku zao, ulaji wa baadhi ya vyakula mfano vyenye viungo vingi, kahawa, nyanya na unga wa ngano.

Kutumia dawa ya meno yenye sodium lauryl sulphate na kuacha kuvuta sigara ghafla, wengi wanaoacha kuvuta sigara kwa mara ya kwanza wanaweza kupatwa na vidonda mdomoni. Chembe za urithi pia zinahusishwa na kupatwa na vidonda mdomoni, angalau asilimia 40 ya watu wanaopatwa na vidonda mdomoni wameripoti kurithi kutoka kwenye familia zao.

Vidonda vya kinywa wakati mwingine husababishwa na magonjwa yanayosababishwa na virusi kama tetekuwanga, magonjwa ya fangasi, magonjwa ya mfumo wa umeng’enyaji wa chakula (Crohn’s Disease, Coeliac Disease), ugonjwa wa kuvimba sehemu za maungio za mwili (Reactive Arthritis), ugonjwa wa kuvimba mishipa ya damu (Behcet’s Disease), kinga ya mwili kudhoofu kutokana na VVU au Lupus, upungufu wa vitamin B na madini chuma.

Pia, Vidonda vya Kinywa vinaweza kusababishwa na matumizi ya dawa mbalimbali kama za kutibu magonjwa mbalimbali mfano kupanda kwa shinikizo la damu na dawa za kutuliza maumivu mfano ibuprofen.

Ninawezaje Kuzuia Vidonda vya Kinywa?

Inaweza kuwa ngumu kuzuia Vidonda vya Kinywa kwa sababu mara nyingi husababishwa na vitu ambavyo huwezi kuvizuia mfano chembe za urithi na maradhi mbalimbali. Ingawa kufanya yafuatayo kunaweza kupunguza hatari ya kupata Vidonda vya Kinywa mfano kuepuka vyakula fulani kama vyenye viungo vingi, kahawa au chokoleti na kula lishe bora.

Epuka kula vyakula vya moto au baridi sana ikiwa una vidonda tayari kwa maana huchelewesha kupona kwa vidonda, kula matunda kwa wingi na mboga za majani ili kuongeza vitamin na madini chuma vitu vinavyoongeza kinga ya mwili, kutotafuna chingamu, kusukutua meno yako na mswaki laini, kutumia dawa ya meno isiyo na sodium lauryl sulphate, kupunguza msongo na wasiwasi.



Post a Comment

Previous Post Next Post