Bakteria wanaweza kuathiri namna unavyojisikia au kuwaza

Bakteria wanaweza kuathiri namna ambavyo tunavyofikiri au kuwaza
Kama kuna kitu chochote kile kinatufanya sisi tuwe binadamu ni fikra ,mawazo na hisia.
Na bado kuna mjadala unaoangalia mtazamo mpya uliojitokeza kudai kwamba bakteria wanaoingia tumboni bila kuonekana wanasababisha athari katika akili zetu.
Sayansi inajumuisha pamoja trilioni ya vijiumbe maradhi ambavyo vinaishi ndani yetu sote na hivyo huathiri afya zetu za kimwili
Lakini hata hivyo hali hii hujumuisha msongo wa mawazo,ugonjwa wa utindio wa ubongo na ugonjwa wa akili ,vyote kwa pamoja vinahusishwa kusababishwa na viumbe hawa vidogo.
Tunajua kwa karne namna ambavyo matumbo yetu yamekuwa yakiathirika,fikiria tu namna ambavyo tumbo linaweza kukuuma kabla ya mtihani au usaili wa kazi lakini sasa ilionekana katika mitazamo miwili tofauti .
Baadhi ya watafiti wanaamini kwamba huu ni wakati wa kufanya mabadiliko ya kutokomeza vimelea vinavyowafanya watu wajisikie hali ya tofauti au kuchanganyikiwa akili na watu kutengemaa kwakuwa na afya nzuri. .

Bakteria wanaweza kuathiri ubongo
Image captionBakteria wanaweza kuathiri ubongo

Watafiti wanaonyesha kwamba bakteria hao huongeza homoni za watu kuwa na msongo wa mawazo.
Utafiti uliofanywa na wanasayansi ukihusisha vimelea vilivyofanyiwa jaribio kwa panya ambao waliokuwa nao na wasiokuwa nao,tabia zao zilikuwaje n ahata namna ambayo ubongo wao ulivyofanya kazi.
Lakini kukuwa kwao ni tofauti kabisa na ulimwengu halisi. Binadamu daima tunawasiliana na viumbe vidogo katika mazingira yetu, hakuna hata mmoja wetu asiye na vijidudu hivi.
Aidha aina ya maisha tunayoisha pia husababisha kuwaamsha hao bakteria,kama vile kutokula mlo kamili au mdogo unatuweka katika mazingira rahisi zaidi ya kuathirika na vimelea hivyo.

Asilimia kubwa ya miili yetu ina vimelea vya maradhi
Image captionAsilimia kubwa ya miili yetu ina bakteria maradhi

Inawezekana kuwa asilimia kubwa ya mwili wako una vimelea hivi vya maradhi ambavyo vinajumuisha bakteria,virusi na fangasi.
Hivyo namna ambavyo hakuna uwiano wa kinga ya mwili na vimelea basi hali ya msongo wa mawazo inaweza kujitokeza na kubadilika kwa tabia.

Vijidudu wanaoingia tumboni wanaweza kusababisha msongo wa mawaz
Image captionVijidudu wanaoingia tumboni husababisha athari katika ubongo

Kuna ushaidi wa awali unaothibitisha uhusishwaji wa vimelea hivyo katika ubongo .
Wataalamu wana nia ya kuwezesha kubadili tabia inayosababisha kuenea kwa ugonjwa huu na kuhamasisha afya njema kwa kila mtu.

Post a Comment

Previous Post Next Post